Msanii mkubwa wa Qaswida hapa Zanzibar Ali ismail kwa sasa anasumbuliwa na maradhi ambayo yamemfanya ashindwe kutembea.
Ali ismail anajulikana sana kwa qaswida zake kama vile
Mkataa kwao mtumwa
Kijungu
Kafara
Safari
Kitendawili
Ali ismail alikua ni miongoni mwa wanafunzi bora pale Al-madrasat Qadiria Amani Zanzibar.
Ali ismail kupitia kurasa zake za tiktok ameweza kushare video inayoonesha akiomba msaada kuhusu maradhi ambayo yanamsibu kwa sasa anahitaji kigari cha kutembelea pia kwa mwenye uwezo wa fedha kuweza kumchangia.
HILI NI LETU SOTE WAPENDA SANAA YA QASWIDA LEO YEYE KESHO SISI.

Hili ni letu sote wana sanaa
ReplyDelete